MAMBO NA WATU
Naja kwenu wanatungo, malenga mulo wachanga, hili neno si uongo, ndio mana nikatunga.
Tusafishe zetu nongo, tusije tukaboronga.
Mambo na watu jamani, mtu lake hataleza.
Mambo na watu jamani, mtu lake hataleza.
Hata ni rahisi kwani, au gumu likikwaza.
Tuwe pamoja gizani, hata mwanga kichomoza.
Mambo na watu sikia, mtu lake hataleza.
Mambo na watu sikia, mtu lake hataleza.
Kujitenga nakwambia, wengine watakukweza.
Shirikio ukitoa, nawe watakuliwaza.
Mambo na watu jamani, mtu lake hataleza.
_*Mfungwa huru*_
Monday, March 12, 2018
TAMBIKO LA AFRIKA
Bara letu afrika, kubwa la pili dunia.
Likambiwa chakarika, mafao kujipatia.
Likapuuza hakika, sasa linajijutia.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Sisi wanaafrika, malofa yulokithiri.
Kwetu mejaa baraka, bado twaitwa fakiri.
Tatizo yote kufika, ujinga meshika ari.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Tukanaitwa kwa majina, nchi zinoendelea.
Kwa sifa tunajivuna, bara salama dunia.
Maendeleo hakuna, twabaki twadidimia.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Pia jina linotisha, bara dunia ya tatu.
Maradhi tunahuisha, kwa ongezeko la watu.
Ya Ebola hatarisha, ukimwi mejaa kwetu.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambikoletu.
Sisemi kwa kulibeza, moyoni ninamachungu.
Iweje wao waweza, sisi tuwe nyuma tangu.
Au ndo tumebatizwa, tusiwe kama wazungu?.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Mfungwa huru
Bara letu afrika, kubwa la pili dunia.
Likambiwa chakarika, mafao kujipatia.
Likapuuza hakika, sasa linajijutia.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Sisi wanaafrika, malofa yulokithiri.
Kwetu mejaa baraka, bado twaitwa fakiri.
Tatizo yote kufika, ujinga meshika ari.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Tukanaitwa kwa majina, nchi zinoendelea.
Kwa sifa tunajivuna, bara salama dunia.
Maendeleo hakuna, twabaki twadidimia.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Pia jina linotisha, bara dunia ya tatu.
Maradhi tunahuisha, kwa ongezeko la watu.
Ya Ebola hatarisha, ukimwi mejaa kwetu.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambikoletu.
Sisemi kwa kulibeza, moyoni ninamachungu.
Iweje wao waweza, sisi tuwe nyuma tangu.
Au ndo tumebatizwa, tusiwe kama wazungu?.
Sisi wanaafrika, hili ndo tambiko letu.
Mfungwa huru
🌷SUBIRI🌷
Habari tumezipata, kuwa yeye aolewa.
Shairi hili matata, wengi litawasumbuwa.
Muwaliko kafumbata, wala hatukuwambiwa.
Pole usihuzunike, simanzi ukajitia.
Hawakukosea watu, maneno kuyatamka.
Kisichoridhiki katu, kwako hakyezi kulika.
Hebu tunza wako utu, ewe mwana msifika.
Maisha safari ndefu, yako ridhiki tapata.
Nilizani zako shere, maneno ulonambia.
Nikayapuuzia bure, sikioni kuyatia.
Mithili kipurepure, upeponi kujongea.
Pole usihuzunike, kumbe kweli aolewa?.
Zimeandikwa mbinguni, ndoa zote na manani.
Usifanye kisirani, ni mtu si hayawani.
Hebu kuwa subirani, utampata mwandani.
Subira subiri chako, mola alokuwekea.
Ituwe akili yako, ipoe na itulie.
Usijefanya vituko, ukaona ujiue.
Yupo wa ridhiki yako, fumba jicho usilie.
Sijui hisia zako, nakuomba vumilia.
Japo alikudanganya, simuwekee kinyongo.
Maneno akakuponya, nawe ukatoa hongo.
Yasahau nakukanya, utakwenda songombingo.
Urafiki ubakie, chuki usimuwekee.
Kutendwa kunaumiza, hilo mimi nalijua.
Mwana nimeshakufunza, ni vyema kusubiria.
Usijeukayabeza, yote niliyokwambia.
Subiri yako ridhiki, mola aloiyandika.
Nimefika kituoni, nanyamaza nisinene.
Jeraha lako moyoni, litibike na lipone.
Usipunguwe mwilini, uzidi wako unene.
Subirini wangu wana, ndoa zimeshaandikwa.
_*by mfungwa huru*_
Habari tumezipata, kuwa yeye aolewa.
Shairi hili matata, wengi litawasumbuwa.
Muwaliko kafumbata, wala hatukuwambiwa.
Pole usihuzunike, simanzi ukajitia.
Hawakukosea watu, maneno kuyatamka.
Kisichoridhiki katu, kwako hakyezi kulika.
Hebu tunza wako utu, ewe mwana msifika.
Maisha safari ndefu, yako ridhiki tapata.
Nilizani zako shere, maneno ulonambia.
Nikayapuuzia bure, sikioni kuyatia.
Mithili kipurepure, upeponi kujongea.
Pole usihuzunike, kumbe kweli aolewa?.
Zimeandikwa mbinguni, ndoa zote na manani.
Usifanye kisirani, ni mtu si hayawani.
Hebu kuwa subirani, utampata mwandani.
Subira subiri chako, mola alokuwekea.
Ituwe akili yako, ipoe na itulie.
Usijefanya vituko, ukaona ujiue.
Yupo wa ridhiki yako, fumba jicho usilie.
Sijui hisia zako, nakuomba vumilia.
Japo alikudanganya, simuwekee kinyongo.
Maneno akakuponya, nawe ukatoa hongo.
Yasahau nakukanya, utakwenda songombingo.
Urafiki ubakie, chuki usimuwekee.
Kutendwa kunaumiza, hilo mimi nalijua.
Mwana nimeshakufunza, ni vyema kusubiria.
Usijeukayabeza, yote niliyokwambia.
Subiri yako ridhiki, mola aloiyandika.
Nimefika kituoni, nanyamaza nisinene.
Jeraha lako moyoni, litibike na lipone.
Usipunguwe mwilini, uzidi wako unene.
Subirini wangu wana, ndoa zimeshaandikwa.
_*by mfungwa huru*_
BILA WEWE
Yaani wewe!, Uliyefanya jina langu likatukuka.
Si mwenginewe, uniokotae pale ninapoanguka.
Na *_bila wewe_*, duniani daima nisingetambulika.
Ndie wewe!, uliyenifanya Tungo nikaiandika.
Si mwenginewe, ila wewe ubongo wangu umeuteka.
Na *_bila wewe_*, furaha yangu duniani ingetoweka.
Haswa! Wewe, uyakosapo mafuta maji hunipaka.
Huna kiwewe nikikukosa hujawahi kasirika.
Na _*bila wewe*_, tabu nyingi nayo mashaka yangenifika.
Ibaki wewe, ninapotukanwa moyo wako huungulika.
Sifa upewe, hujawahi nibagua katika kila rika.
Na *_bila wewe_*, nisingelijua lipi jema la kushika.
_*by Ochu*_
_*Mfungwa huru*_
Yaani wewe!, Uliyefanya jina langu likatukuka.
Si mwenginewe, uniokotae pale ninapoanguka.
Na *_bila wewe_*, duniani daima nisingetambulika.
Ndie wewe!, uliyenifanya Tungo nikaiandika.
Si mwenginewe, ila wewe ubongo wangu umeuteka.
Na *_bila wewe_*, furaha yangu duniani ingetoweka.
Haswa! Wewe, uyakosapo mafuta maji hunipaka.
Huna kiwewe nikikukosa hujawahi kasirika.
Na _*bila wewe*_, tabu nyingi nayo mashaka yangenifika.
Ibaki wewe, ninapotukanwa moyo wako huungulika.
Sifa upewe, hujawahi nibagua katika kila rika.
Na *_bila wewe_*, nisingelijua lipi jema la kushika.
_*by Ochu*_
_*Mfungwa huru*_
Saturday, March 10, 2018
💞VITA VINATUANDAMA💞
Naanza kutakalamu, kuyasema kwenu umma.
Akili yangu timamu, inafanya kazi vyema.
Si chizi si mwendazimu, kiafya nipo mzima.
NAWAZINDUA MAPEMA, VITA VINATUANDAMA.
Kupambana ni wajibu, vita vinapoingia.
Kwa peni nacho kitabu, silaha mwazitambua.
Mabomu yakughilibu, vifaru mizinga pia.
SASA SOTE TUAMKE, VITA VINATUANDAMA.
Tusijefanya ajizi, tukaja kupuuzia.
Hivi si vya mapinduzi, wala vile vya dunia.
Tujiandae kikazi, tuweze kujiokoa.
VITA NASEMA MAPEMA, VITA VINATUANDAMA.
Adui kimpa njaa, vita kwako huwa vyema.
Atajawa na fadhaa, tutashinda himahima.
Naona mmeduwaa, mbona hamjasimama?.
SASA VINAKARIBIA, TUJIANDAE KIUME.
Vita sasa vimefika, adui tumkabili.
Tena bila ya kuchoka, tupigane kikatili.
Nguvu pamoja hakika, najaha itawasili.
MBONA HAMJAZINDUKA?, VITA SASA VIMEFIKA.
Hapa naweka kituo, nisijevuka mipaka.
Nikawa nnazo nguo, ila sijasitirika.
Kwani langu kumbushio, tayari limeshafika.
TUAMKE TUAMKE, VITA SASA VIMEFIKA.
🌷BY OCHU🌷
📢📢📢Mfungwa huru📢📢📢
Naanza kutakalamu, kuyasema kwenu umma.
Akili yangu timamu, inafanya kazi vyema.
Si chizi si mwendazimu, kiafya nipo mzima.
NAWAZINDUA MAPEMA, VITA VINATUANDAMA.
Kupambana ni wajibu, vita vinapoingia.
Kwa peni nacho kitabu, silaha mwazitambua.
Mabomu yakughilibu, vifaru mizinga pia.
SASA SOTE TUAMKE, VITA VINATUANDAMA.
Tusijefanya ajizi, tukaja kupuuzia.
Hivi si vya mapinduzi, wala vile vya dunia.
Tujiandae kikazi, tuweze kujiokoa.
VITA NASEMA MAPEMA, VITA VINATUANDAMA.
Adui kimpa njaa, vita kwako huwa vyema.
Atajawa na fadhaa, tutashinda himahima.
Naona mmeduwaa, mbona hamjasimama?.
SASA VINAKARIBIA, TUJIANDAE KIUME.
Vita sasa vimefika, adui tumkabili.
Tena bila ya kuchoka, tupigane kikatili.
Nguvu pamoja hakika, najaha itawasili.
MBONA HAMJAZINDUKA?, VITA SASA VIMEFIKA.
Hapa naweka kituo, nisijevuka mipaka.
Nikawa nnazo nguo, ila sijasitirika.
Kwani langu kumbushio, tayari limeshafika.
TUAMKE TUAMKE, VITA SASA VIMEFIKA.
🌷BY OCHU🌷
📢📢📢Mfungwa huru📢📢📢
🌷WASIFAZO SIMPATI🌷
Hali yangu niko fiti, mzima wa afya pia.
Naiomba hidayati, mola niongoze njia.
Pia nyingi hasanati, za akhera na dunia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Uzuri wako banati, weupe wa asilia.
Na wekundu samawati, maji kunde mithilia.
Tabia zako thabiti, vyote vimenivutia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Punguza uafiriti, yangu kauli sikia.
Nikuonapo sijuti, moyo wangu hutulia.
Kwako raha mi sipati, machoni sipokutia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Mambo yapo jaharati, tena unayatambua.
Kuwa kwako nimeketi, moyo nimekuachia.
Uendapo udhibiti, ruhusa mekupatia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Upendo wangu wa dhati, kidondani meozea.
Kwako niko mahatuti, wewe wa kuniokoa.
Kama kwako si bahati, ujue nitajiua.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Nimefikia tamati, shairi namalizia.
Pendo lako ni bahati, kamwe sitalichezea.
Nitaomba ghufirati, pale nikikukosea.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
🌷by ochu🌷
MFUNGWA HURU
Hali yangu niko fiti, mzima wa afya pia.
Naiomba hidayati, mola niongoze njia.
Pia nyingi hasanati, za akhera na dunia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Uzuri wako banati, weupe wa asilia.
Na wekundu samawati, maji kunde mithilia.
Tabia zako thabiti, vyote vimenivutia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Punguza uafiriti, yangu kauli sikia.
Nikuonapo sijuti, moyo wangu hutulia.
Kwako raha mi sipati, machoni sipokutia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Mambo yapo jaharati, tena unayatambua.
Kuwa kwako nimeketi, moyo nimekuachia.
Uendapo udhibiti, ruhusa mekupatia.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Upendo wangu wa dhati, kidondani meozea.
Kwako niko mahatuti, wewe wa kuniokoa.
Kama kwako si bahati, ujue nitajiua.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
Nimefikia tamati, shairi namalizia.
Pendo lako ni bahati, kamwe sitalichezea.
Nitaomba ghufirati, pale nikikukosea.
Wasifazo simpati, nitamaliza dunia.
🌷by ochu🌷
MFUNGWA HURU
BADO HAMJABWABWAJA
Kila muda vikundini, midomoni kututia.
Tushuke zetu thamani, hili tumeshitukia.
Kusengenya namba wani, kuropokwa mezoea.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Si mipasho ikhiwani, ujumbe kwenu twatoa.
Tumechoka kwa yakini, ila tunavumilia.
Maji kitia katani, yakogee sije poa
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Tumetia akilini, maneno munorongoa.
Ila siyapi imani, kwetu yanatuchefua.
Wanazusha tafrani, ugomvi kuuibua.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Wazidi chochea kuni, moto uzidi kolea.
Kuyazua yetu kwani, hili halijasumbua.
Tunang'ara izirani, kama miale ya jua.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Mwabwabwaja hadharani, thamani zetu kutoa.
Kuwambia wafulani, ndiko munaabudia.
Hatushughuliki kwani, yetu yanatuendea.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Beti sita uwanjani, zitoshe kuwaambia.
Kubwabwaja toshekeni, muda wenu wapotea.
Kutusema vikundini, kwikwi zitawapalia.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
*_By ochu_*
*_Mfungwa huru_*
Kila muda vikundini, midomoni kututia.
Tushuke zetu thamani, hili tumeshitukia.
Kusengenya namba wani, kuropokwa mezoea.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Si mipasho ikhiwani, ujumbe kwenu twatoa.
Tumechoka kwa yakini, ila tunavumilia.
Maji kitia katani, yakogee sije poa
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Tumetia akilini, maneno munorongoa.
Ila siyapi imani, kwetu yanatuchefua.
Wanazusha tafrani, ugomvi kuuibua.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Wazidi chochea kuni, moto uzidi kolea.
Kuyazua yetu kwani, hili halijasumbua.
Tunang'ara izirani, kama miale ya jua.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Mwabwabwaja hadharani, thamani zetu kutoa.
Kuwambia wafulani, ndiko munaabudia.
Hatushughuliki kwani, yetu yanatuendea.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
Beti sita uwanjani, zitoshe kuwaambia.
Kubwabwaja toshekeni, muda wenu wapotea.
Kutusema vikundini, kwikwi zitawapalia.
Bado hamjabwabwaja, zidisheni nawambia.
*_By ochu_*
*_Mfungwa huru_*
SEMA YANOUSHUHUDA
Naja kutia mkazo, kwa lile nilowambia.
Ila lisiwe tatizo, kukwaza wapita njia.
Yanoushuhuda mwanzo, yesema kiyapania.
Usiropokwe kijinga, ukome wako ulimi.
Sasa mmezidi mno, wezenu kufatilia.
Kazi yenu minong'ono, ya kwao kusimulia.
Ishara na kwa mifano, na mafumbo kutumia.
Usiropokwe kijinga, ukome wako ulimi.
Sijakwambia bwabwaja, kusema soshuhudia.
Au watu kuwataja, majina kuchafulia.
Ila uzitoe hoja, kwa ulioshuhudia.
Usibwabwaje kijinga, ikome yako midomo.
Sikuja kuwakomesha, natoa yenye udhia.
Ili mambo kuboresha, ya kwetu kufatilia.
Laleni au kukesha, msile msinywe pia.
*_Ila_*
Sema yanoushuhuda, siseme ya kusikia.
Naanza na Taimuri, umbea mekuzidia.
Zingatia ushauri, soyajua ulizia.
Usibwabwaje dhahiri, ya watu kuhadithia.
Sema yanoushuda, siseme ya kusikia.
Naungulia moyoni, Dillah wewe kukwambia,
Hashimu na da Mgeni, heshima nawapatia.
Ila haya yashikeni, yote niliowambia.
Sema yanoushuhuda, watu watakuelewa.
Na isiwe mada kesi, mpole sitomwambia.
Luti simwage kamasi, usoni kunirushia.
Kwake Bimu sina wasi, lakini namuwambia.
Siropokwe soyajua, yatakuja kukuponza.
Wahida yeye mbishi, haya atapuuzia.
Ataleta magumashi, na hata kuninunia.
Ila haliniyumbishi, ngangari nitabakia.
Sema yanoushuhuda, siseme usoyajua.
Khadija tunao wengi, kimya wamejikalia.
Hii sifa ya msingi, mola kawatunukia.
Kwao kubwabwaja kwingi, wameshajizuilia.
*_Ila_*
Pale mtapobwabwaja, sema yanoushuhuda.
Nachukua kihanjifu, majasho ninafutia.
Arafa sijekashifu, eti nakufatilia.
Sijaja humu kwa rafu, ugomvi kufuatia.
Mdomo wako uchunge, usije ukakuponza.
Mwisho kwa Mimi mtunzi, Ochu sijakamilia.
Wengi walinita tozi, jina kunichafulia.
Sifa yangu kurumbwizi, zuri shida kinijia.
Kibaya kwangu kichaka, pale nikijitokea.
Ila nikome kusema ovyo, Yale nisoshuhudia.
By Mfungwa huru
Naja kutia mkazo, kwa lile nilowambia.
Ila lisiwe tatizo, kukwaza wapita njia.
Yanoushuhuda mwanzo, yesema kiyapania.
Usiropokwe kijinga, ukome wako ulimi.
Sasa mmezidi mno, wezenu kufatilia.
Kazi yenu minong'ono, ya kwao kusimulia.
Ishara na kwa mifano, na mafumbo kutumia.
Usiropokwe kijinga, ukome wako ulimi.
Sijakwambia bwabwaja, kusema soshuhudia.
Au watu kuwataja, majina kuchafulia.
Ila uzitoe hoja, kwa ulioshuhudia.
Usibwabwaje kijinga, ikome yako midomo.
Sikuja kuwakomesha, natoa yenye udhia.
Ili mambo kuboresha, ya kwetu kufatilia.
Laleni au kukesha, msile msinywe pia.
*_Ila_*
Sema yanoushuhuda, siseme ya kusikia.
Naanza na Taimuri, umbea mekuzidia.
Zingatia ushauri, soyajua ulizia.
Usibwabwaje dhahiri, ya watu kuhadithia.
Sema yanoushuda, siseme ya kusikia.
Naungulia moyoni, Dillah wewe kukwambia,
Hashimu na da Mgeni, heshima nawapatia.
Ila haya yashikeni, yote niliowambia.
Sema yanoushuhuda, watu watakuelewa.
Na isiwe mada kesi, mpole sitomwambia.
Luti simwage kamasi, usoni kunirushia.
Kwake Bimu sina wasi, lakini namuwambia.
Siropokwe soyajua, yatakuja kukuponza.
Wahida yeye mbishi, haya atapuuzia.
Ataleta magumashi, na hata kuninunia.
Ila haliniyumbishi, ngangari nitabakia.
Sema yanoushuhuda, siseme usoyajua.
Khadija tunao wengi, kimya wamejikalia.
Hii sifa ya msingi, mola kawatunukia.
Kwao kubwabwaja kwingi, wameshajizuilia.
*_Ila_*
Pale mtapobwabwaja, sema yanoushuhuda.
Nachukua kihanjifu, majasho ninafutia.
Arafa sijekashifu, eti nakufatilia.
Sijaja humu kwa rafu, ugomvi kufuatia.
Mdomo wako uchunge, usije ukakuponza.
Mwisho kwa Mimi mtunzi, Ochu sijakamilia.
Wengi walinita tozi, jina kunichafulia.
Sifa yangu kurumbwizi, zuri shida kinijia.
Kibaya kwangu kichaka, pale nikijitokea.
Ila nikome kusema ovyo, Yale nisoshuhudia.
By Mfungwa huru
YAMENIFIKA
Mwezenu yamenifika, sikieni.
Hili jambo uhakika, bwabwajeni.
Nampenda kihakika, bi fulani.
Jina sikutajieni.
Chuoni hajapafika, msibuni.
Mkaanza paparka, ni Fulani.
Nampenda pasi shaka, ni mwandani.
Daima sitomuwacha.
Hilo munolitamka, ni uhuni.
Sio kila linozuka, midomoni.
Kuwa ndilo uhakika, fikirini.
Kabla ya kubwabwaja.
By Mfungwa huru
Mwezenu yamenifika, sikieni.
Hili jambo uhakika, bwabwajeni.
Nampenda kihakika, bi fulani.
Jina sikutajieni.
Chuoni hajapafika, msibuni.
Mkaanza paparka, ni Fulani.
Nampenda pasi shaka, ni mwandani.
Daima sitomuwacha.
Hilo munolitamka, ni uhuni.
Sio kila linozuka, midomoni.
Kuwa ndilo uhakika, fikirini.
Kabla ya kubwabwaja.
By Mfungwa huru
CHANGAMOTO NDO MAISHA
Naja tena kwa unyonge, kundini kuwakumbusha.
Mambo wazi nisifunge, ujumbe kuufikisha.
Yawaondoke mazonge, rohoni yanowarusha.
Hutoweza fanikiwa, bila kupata mazito.
Changamoto duniani, zipo pia zinafunza.
Zawafika insani, akili zao kukuza.
Watu sio punguwani, badala huzigeuza.
Ukijua changamoto, fanikio tatakuja.
Bila shaka hula mbivu, yule atovumilia.
Kuwacha wake uvivu, maarifa kutumia.
Pia kiwa muangavu, kwa mambo yalomjia.
Subira nguo adhima, ikiivaa hujuti.
Maneno sio mkuki, usiyajali ya watu.
Adui sio rafiki, akulae kama chatu.
Sisadiki wanafiki, kwao hutapat kitu.
Vazi la mtu tabia, utu si sura sikia.
Changamoto ninasema, shida tabu matatizo.
Iweke subira njema, itoe yako mizozo.
Ngangari simama wima, maisha ndo lako funzo.
Njia za mafanikio, changamoto na subira.
Sita beti zimetimu, inatosha kuhubiri.
Subira kitu muhimu, usijifanye jabari.
Usije kunilaumu, tayari 'shakupa siri.
*_TENA_*
Sio kila ufanyalo, wengi litawavutia.
By mfungwa huru
Naja tena kwa unyonge, kundini kuwakumbusha.
Mambo wazi nisifunge, ujumbe kuufikisha.
Yawaondoke mazonge, rohoni yanowarusha.
Hutoweza fanikiwa, bila kupata mazito.
Changamoto duniani, zipo pia zinafunza.
Zawafika insani, akili zao kukuza.
Watu sio punguwani, badala huzigeuza.
Ukijua changamoto, fanikio tatakuja.
Bila shaka hula mbivu, yule atovumilia.
Kuwacha wake uvivu, maarifa kutumia.
Pia kiwa muangavu, kwa mambo yalomjia.
Subira nguo adhima, ikiivaa hujuti.
Maneno sio mkuki, usiyajali ya watu.
Adui sio rafiki, akulae kama chatu.
Sisadiki wanafiki, kwao hutapat kitu.
Vazi la mtu tabia, utu si sura sikia.
Changamoto ninasema, shida tabu matatizo.
Iweke subira njema, itoe yako mizozo.
Ngangari simama wima, maisha ndo lako funzo.
Njia za mafanikio, changamoto na subira.
Sita beti zimetimu, inatosha kuhubiri.
Subira kitu muhimu, usijifanye jabari.
Usije kunilaumu, tayari 'shakupa siri.
*_TENA_*
Sio kila ufanyalo, wengi litawavutia.
By mfungwa huru
NJIWA ASOHURUMA
Njiwa kwangu katuwa, kilipo chagu kidonda.
Kidonda chataka sawa, afurahi nikikonda.
Kanipiga lake bawa, pale kilipo kidonda.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli kanitonesha.
Siku ya pili akaja, na hasira nyingi sana.
Kanipiga dono moja, dono lino kubwa sana.
Damu ikaanza vuja, kweli anitesa sana.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Dawa yangu ipo kwake, anajuwa kwa undani.
Kikweli mateso yake, ni kama ya hayawani.
Ila kusudio lake, kunitia mtihani.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Siku nyingi zikapita, na miezi kujongea.
Dawa nikaitafuta, ila sijaivumbua.
Nikabaki nnatuta, pumzi za mwisho kutoa.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Nikapoteza uhai, kwa yote yake mashaka.
Njiwa kweli ni adui, kaburini kaniweka.
Nikazikwa niko hai, tena njiwa karidhika.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli kafanikiwa.
_*by ochu*_
_*mfungwa huru*_
Njiwa kwangu katuwa, kilipo chagu kidonda.
Kidonda chataka sawa, afurahi nikikonda.
Kanipiga lake bawa, pale kilipo kidonda.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli kanitonesha.
Siku ya pili akaja, na hasira nyingi sana.
Kanipiga dono moja, dono lino kubwa sana.
Damu ikaanza vuja, kweli anitesa sana.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Dawa yangu ipo kwake, anajuwa kwa undani.
Kikweli mateso yake, ni kama ya hayawani.
Ila kusudio lake, kunitia mtihani.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Siku nyingi zikapita, na miezi kujongea.
Dawa nikaitafuta, ila sijaivumbua.
Nikabaki nnatuta, pumzi za mwisho kutoa.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli anitonesha.
Nikapoteza uhai, kwa yote yake mashaka.
Njiwa kweli ni adui, kaburini kaniweka.
Nikazikwa niko hai, tena njiwa karidhika.
Njiwa asonahuruma, kwa kweli kafanikiwa.
_*by ochu*_
_*mfungwa huru*_
MFUNGWA HURU
Naja kwenu kwa unyonge, kueleza yanosibu.
Mistari niipange, na vina vyastahabu.
Kibwagizo nikifunge, kwa neno lenye ajabu.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Kua mwana utaona, niliambiwa zamani.
Usayaona mchana, utayaona gizani.
Dunia wanja wa lana, kweli sasa mebaini.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Dudia sasa yatisha, vitendovye hayawani.
Mambo yanoatilisha, hayo mejaa pomoni.
Si kama namaanisha, kukosoa kudurani.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Duniani kuna watu, waliotaalamika.
Wanotengeza mitutu, na mabomu kadhalika.
Ili kuulia watu, ulinzi pia kuweka.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Eti ni maendeleo, kuigawanya mipaka.
Ya dunia midenguo, isijekukuachika.
Utaitafuta ngao, ushindwe pakwenda shika.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Dunia kama kijiji, watu wamekigeuza.
Sio nchi wala miji, wote wamejitandaza.
Sio tu kupiga maji, neno chafu kucharaza.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Yale yanonishangaza, kufumbua mboni zangu.
Nikiona chapendeza, kumbe pia ni kichungu.
Mapenzi yaniburuza, kweli hii jela chungu.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Ukingalia kwa kina, utaona yapendeza.
Mapambo kila aina yaliyojilimbikiza.
Usiku kama mchana, kweli hii miujiza.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Kila nikisonga mbele, nafsi inanitetema.
Kutoa zangu kelele, moyoni wanisakama.
Wanataka niwe kule, enzi za baba na mama.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Nakuomba uzinduke, mwana wa kidigitali.
Hali yangu ikumbuke, ilivyokuwa dhalili.
Vituko anasa zake, jela hii ni katili.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
*_by mfungwa huru_*
Naja kwenu kwa unyonge, kueleza yanosibu.
Mistari niipange, na vina vyastahabu.
Kibwagizo nikifunge, kwa neno lenye ajabu.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Kua mwana utaona, niliambiwa zamani.
Usayaona mchana, utayaona gizani.
Dunia wanja wa lana, kweli sasa mebaini.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Dudia sasa yatisha, vitendovye hayawani.
Mambo yanoatilisha, hayo mejaa pomoni.
Si kama namaanisha, kukosoa kudurani.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Duniani kuna watu, waliotaalamika.
Wanotengeza mitutu, na mabomu kadhalika.
Ili kuulia watu, ulinzi pia kuweka.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Eti ni maendeleo, kuigawanya mipaka.
Ya dunia midenguo, isijekukuachika.
Utaitafuta ngao, ushindwe pakwenda shika.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Dunia kama kijiji, watu wamekigeuza.
Sio nchi wala miji, wote wamejitandaza.
Sio tu kupiga maji, neno chafu kucharaza.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Yale yanonishangaza, kufumbua mboni zangu.
Nikiona chapendeza, kumbe pia ni kichungu.
Mapenzi yaniburuza, kweli hii jela chungu.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Ukingalia kwa kina, utaona yapendeza.
Mapambo kila aina yaliyojilimbikiza.
Usiku kama mchana, kweli hii miujiza.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Kila nikisonga mbele, nafsi inanitetema.
Kutoa zangu kelele, moyoni wanisakama.
Wanataka niwe kule, enzi za baba na mama.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
Nakuomba uzinduke, mwana wa kidigitali.
Hali yangu ikumbuke, ilivyokuwa dhalili.
Vituko anasa zake, jela hii ni katili.
Mimi ni mfungwa huru, dunia ndio gereza.
*_by mfungwa huru_*
DONGE
Siambi mimi hodari, wanatungo mwatambua.
Wala sitafuti shari, shairi kulitungia.
Ila neka hafikiri, wazo lililonijia.
Ipi maana sahili, ya neno *_donge_* jamia.
Yahangaika suduri, majibu kutafutia.
Maana ilo shuwari, ya neno donge jamia.
Nami bila ya hiari, leo ninaulizia.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge naweka rohoni, nyongo inaponibana.
Donge machungu moyoni, utaponikera sana.
Donge ni fundo kooni, kinikera nakuchana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni zonge la uzi, lililozongwa vizuri.
Kwa kireli kilowazi, na madhubuti hatari.
Kizongoa huwa kazi, usipokuwa mahari.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge pia ni finyango, yabisi ni yake hali.
Donge finyango la dongo, lilosokotwa sahali.
Donge dawa si uongo, kwa maradhi mbalimbali.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge la chumvi jamani, hili nalo tutambue.
Donge halina thamani, shimmia uuziwe.
Donge hutiwa chunguni, chakulani likolee.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ndani mna nini?, mana limesokotana.
Donge lina siri gani, mbona mnalitukana.
Donge liko taabani, mapande limeachana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni kijiji chema, kwao baba nae mama.
Donge mejaa neema, kairuzuku karima.
Donge nasema salama, ugomvi sio heshima.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ninaweka tama, mbele sitoendelea.
Donge nimeshasimama, majibu kusubiria.
Nyote na mufanye hima, sudurini weze poa.
Ipi maana halisi, neno *_donge_* jamia.
_*by mfungwa huru*_
Siambi mimi hodari, wanatungo mwatambua.
Wala sitafuti shari, shairi kulitungia.
Ila neka hafikiri, wazo lililonijia.
Ipi maana sahili, ya neno *_donge_* jamia.
Yahangaika suduri, majibu kutafutia.
Maana ilo shuwari, ya neno donge jamia.
Nami bila ya hiari, leo ninaulizia.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge naweka rohoni, nyongo inaponibana.
Donge machungu moyoni, utaponikera sana.
Donge ni fundo kooni, kinikera nakuchana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni zonge la uzi, lililozongwa vizuri.
Kwa kireli kilowazi, na madhubuti hatari.
Kizongoa huwa kazi, usipokuwa mahari.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge pia ni finyango, yabisi ni yake hali.
Donge finyango la dongo, lilosokotwa sahali.
Donge dawa si uongo, kwa maradhi mbalimbali.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge la chumvi jamani, hili nalo tutambue.
Donge halina thamani, shimmia uuziwe.
Donge hutiwa chunguni, chakulani likolee.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ndani mna nini?, mana limesokotana.
Donge lina siri gani, mbona mnalitukana.
Donge liko taabani, mapande limeachana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni kijiji chema, kwao baba nae mama.
Donge mejaa neema, kairuzuku karima.
Donge nasema salama, ugomvi sio heshima.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ninaweka tama, mbele sitoendelea.
Donge nimeshasimama, majibu kusubiria.
Nyote na mufanye hima, sudurini weze poa.
Ipi maana halisi, neno *_donge_* jamia.
_*by mfungwa huru*_
Siambi mimi hodari, wanatungo mwatambua.
Wala sitafuti shari, shairi kulitungia.
Ila neka hafikiri, wazo lililonijia.
Ipi maana sahili, ya neno *_donge_* jamia.
Yahangaika suduri, majibu kutafutia.
Maana ilo shuwari, ya neno donge jamia.
Nami bila ya hiari, leo ninaulizia.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge naweka rohoni, nyongo inaponibana.
Donge machungu moyoni, utaponikera sana.
Donge ni fundo kooni, kinikera nakuchana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni zonge la uzi, lililozongwa vizuri.
Kwa kireli kilowazi, na madhubuti hatari.
Kizongoa huwa kazi, usipokuwa mahari.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge pia ni finyango, yabisi ni yake hali.
Donge finyango la dongo, lilosokotwa sahali.
Donge dawa si uongo, kwa maradhi mbalimbali.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge la chumvi jamani, hili nalo tutambue.
Donge halina thamani, shimmia uuziwe.
Donge hutiwa chunguni, chakulani likolee.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ndani mna nini?, mana limesokotana.
Donge lina siri gani, mbona mnalitukana.
Donge liko taabani, mapande limeachana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni kijiji chema, kwao baba nae mama.
Donge mejaa neema, kairuzuku karima.
Donge nasema salama, ugomvi sio heshima.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ninaweka tama, mbele sitoendelea.
Donge nimeshasimama, majibu kusubiria.
Nyote na mufanye hima, sudurini weze poa.
Ipi maana halisi, neno *_donge_* jamia.
_*by mfungwa huru*_
Siambi mimi hodari, wanatungo mwatambua.
Wala sitafuti shari, shairi kulitungia.
Ila neka hafikiri, wazo lililonijia.
Ipi maana sahili, ya neno *_donge_* jamia.
Yahangaika suduri, majibu kutafutia.
Maana ilo shuwari, ya neno donge jamia.
Nami bila ya hiari, leo ninaulizia.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge naweka rohoni, nyongo inaponibana.
Donge machungu moyoni, utaponikera sana.
Donge ni fundo kooni, kinikera nakuchana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni zonge la uzi, lililozongwa vizuri.
Kwa kireli kilowazi, na madhubuti hatari.
Kizongoa huwa kazi, usipokuwa mahari.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge pia ni finyango, yabisi ni yake hali.
Donge finyango la dongo, lilosokotwa sahali.
Donge dawa si uongo, kwa maradhi mbalimbali.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge la chumvi jamani, hili nalo tutambue.
Donge halina thamani, shimmia uuziwe.
Donge hutiwa chunguni, chakulani likolee.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ndani mna nini?, mana limesokotana.
Donge lina siri gani, mbona mnalitukana.
Donge liko taabani, mapande limeachana.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ni kijiji chema, kwao baba nae mama.
Donge mejaa neema, kairuzuku karima.
Donge nasema salama, ugomvi sio heshima.
Ipi maana halisi, ya neno *_donge_* jamia.
Donge ninaweka tama, mbele sitoendelea.
Donge nimeshasimama, majibu kusubiria.
Nyote na mufanye hima, sudurini weze poa.
Ipi maana halisi, neno *_donge_* jamia.
_*by mfungwa huru*_
***KIGENGE***
1)Huu wangu mtazamo, nionavyo nawambia. Hisia ziumoumo, nihisivyo nazitoa. eti ni mdogo kimo, na miaka mtazua. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
2) Watasema siyajui, yaliotokea nyuma. waliuwa maadui, kigenge kikasimama. Ila sasa hakifai, kinatukondesha nyama. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti.
3) Kigenge hicho sikia, wizi wa kupindukia. shitaka ukifungua, hongo wanahitajia. Bangi unga huingia, bila ya kuwazuia. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
4)Sikichukii kigenge, ila siwapendi watu. Wala sipendi kigenge, bali nawapenda watu. Wanaojali wanyonge, kuthamini wao utu. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti.
5) Kigenge kipo zamani, enzi zile za mababu. sasa hakina thamani, kimetutoka muhibu. Waongezeka wahuni, ukweli twapata tabu. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
6) Kigenge mbona si shwari, kinahodhi mali zetu. sasa kikirikikiri, tunamwaga damu zete. Kwa bongo na ujasiri, kurejesha utu wetu. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti
7)Mwisho nanena kigenge, tukiroge uchawini. Gerezani tukifunge, kisitoke abadani. sote pamoja wanyonge, tutashinda kwa imani. Kigenge tukiondoe, wahuni wamalizike...
Mtunzi: Othman Ame Hamza.
Lakabu: Mfungwa huru [Free prisoner]
Mshairi wa Donge...
Tel:0776820608
HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA
1)Huu wangu mtazamo, nionavyo nawambia. Hisia ziumoumo, nihisivyo nazitoa. eti ni mdogo kimo, na miaka mtazua. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
2) Watasema siyajui, yaliotokea nyuma. waliuwa maadui, kigenge kikasimama. Ila sasa hakifai, kinatukondesha nyama. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti.
3) Kigenge hicho sikia, wizi wa kupindukia. shitaka ukifungua, hongo wanahitajia. Bangi unga huingia, bila ya kuwazuia. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
4)Sikichukii kigenge, ila siwapendi watu. Wala sipendi kigenge, bali nawapenda watu. Wanaojali wanyonge, kuthamini wao utu. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti.
5) Kigenge kipo zamani, enzi zile za mababu. sasa hakina thamani, kimetutoka muhibu. Waongezeka wahuni, ukweli twapata tabu. Kigenge kimetubana, ngama yatutoka nyuma.
6) Kigenge mbona si shwari, kinahodhi mali zetu. sasa kikirikikiri, tunamwaga damu zete. Kwa bongo na ujasiri, kurejesha utu wetu. Kigenge kimetubana, wala hatufurukuti
7)Mwisho nanena kigenge, tukiroge uchawini. Gerezani tukifunge, kisitoke abadani. sote pamoja wanyonge, tutashinda kwa imani. Kigenge tukiondoe, wahuni wamalizike...
Mtunzi: Othman Ame Hamza.
Lakabu: Mfungwa huru [Free prisoner]
Mshairi wa Donge...
Tel:0776820608
HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA
Monday, March 5, 2018
WASIA WA BABU
Babu kabla ya kufa, usia kunipatia.
Kwamba dunia maafa, nikae kuzingatia.
Akanipa zake sifa, Nzuri na mbaya pia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Duniani yapo mengi, alianza nihusia.
Aliyapaka na rangi, mazuri alonambia.
Ila jambo la msingi, niweze yazingatia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Pia alinihusia, dunia ina anasa.
Usije kuzipania, sikia ninakuasa.
Wengi walishapotea, kisingizio siasa.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Sikio alinishika, ataka nizingatie.
Kukaa na Kila rika, wala nisizibague.
Ila pazuri kushika, penye kwendana na mie.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Aliingiwa na hari, nikawa nampepea.
Akanza tahayari, na sana kunihofia.
Mithili maji bahari, machozi aliyatoa.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Alinihusia mengi, niepuke marafiki.
Wale wavutaji bangi, na wanao kunywa arki.
Hata wale mashangingi, bure watakuhilaki.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Mwisho alinihusia, dunia ni kama njia.
Kaa na waja kwa nia, njema isiyoudhia.
Shida wakikuletea, waweza wasaidia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
_*By ochu*_
_*Mfungwa huru*_
NAKIREJEA KIMEO
Naja mbele ya umati, naandika kusudio.
Naililia bahati, niko hoi mbiombio.
Taabani mahatuti, zinipungue hashuo.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Dharau zimeniponza, kimeo kukifutuka.
Na sasa nimejifunza, kimeo kina baraka.
Hizi kubwa zaumiza, zaunguza ukishika.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Simu kubwa zao hao, wakubwa wenye na vyao.
Au pia mabishoo, wanouza sura zao.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Bora kimeo cha jadi, tabu kwake sijapata.
Chaji natumia hadi, Masiku bila utata.
Nikichaji pasi kedi, kinajaa fastafasta.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Kubwa zina mambo mengi, simu hizi za kisasa.
Utachaji mara nyingi, siku moja mara tisa.
Matumizi siyapingi, kama jicho ukipwesa.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Yanitia mashakani, simu ya androidi.
Simati foni si shani, mobaili ufisadi.
Kimeo kimfukoni, si kimoto kibaridi.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Simu kubwa kuilinda, gadi inahitajia.
Hushuka Mara hupanda, mnara unasumbua.
Ikidondoka varanda, siyako nakuambia.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Nakirejea kimeo, simatifoni yatesa.
Haya mambo ya kileo, bora niwe nayakosa.
Kila usiku uchao, uwe mpya ukurasa.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Beti tisa zinatosha, nakirejea kimeo.
Hizi kubwa zakondesha, kimeo chanipa ngao.
Kimeo kwangu bashasha, hakihitaji mafao.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
*_BY OCHU_*
*_mfungwa huru_*
Babu kabla ya kufa, usia kunipatia.
Kwamba dunia maafa, nikae kuzingatia.
Akanipa zake sifa, Nzuri na mbaya pia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Duniani yapo mengi, alianza nihusia.
Aliyapaka na rangi, mazuri alonambia.
Ila jambo la msingi, niweze yazingatia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Pia alinihusia, dunia ina anasa.
Usije kuzipania, sikia ninakuasa.
Wengi walishapotea, kisingizio siasa.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Sikio alinishika, ataka nizingatie.
Kukaa na Kila rika, wala nisizibague.
Ila pazuri kushika, penye kwendana na mie.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Aliingiwa na hari, nikawa nampepea.
Akanza tahayari, na sana kunihofia.
Mithili maji bahari, machozi aliyatoa.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Alinihusia mengi, niepuke marafiki.
Wale wavutaji bangi, na wanao kunywa arki.
Hata wale mashangingi, bure watakuhilaki.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
Mwisho alinihusia, dunia ni kama njia.
Kaa na waja kwa nia, njema isiyoudhia.
Shida wakikuletea, waweza wasaidia.
Usia wake daima, kamwe sitausahau.
_*By ochu*_
_*Mfungwa huru*_
NAKIREJEA KIMEO
Naja mbele ya umati, naandika kusudio.
Naililia bahati, niko hoi mbiombio.
Taabani mahatuti, zinipungue hashuo.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Dharau zimeniponza, kimeo kukifutuka.
Na sasa nimejifunza, kimeo kina baraka.
Hizi kubwa zaumiza, zaunguza ukishika.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Simu kubwa zao hao, wakubwa wenye na vyao.
Au pia mabishoo, wanouza sura zao.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Bora kimeo cha jadi, tabu kwake sijapata.
Chaji natumia hadi, Masiku bila utata.
Nikichaji pasi kedi, kinajaa fastafasta.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Kubwa zina mambo mengi, simu hizi za kisasa.
Utachaji mara nyingi, siku moja mara tisa.
Matumizi siyapingi, kama jicho ukipwesa.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Yanitia mashakani, simu ya androidi.
Simati foni si shani, mobaili ufisadi.
Kimeo kimfukoni, si kimoto kibaridi.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Simu kubwa kuilinda, gadi inahitajia.
Hushuka Mara hupanda, mnara unasumbua.
Ikidondoka varanda, siyako nakuambia.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Nakirejea kimeo, simatifoni yatesa.
Haya mambo ya kileo, bora niwe nayakosa.
Kila usiku uchao, uwe mpya ukurasa.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
Beti tisa zinatosha, nakirejea kimeo.
Hizi kubwa zakondesha, kimeo chanipa ngao.
Kimeo kwangu bashasha, hakihitaji mafao.
Sitoacha m-bachao, nakirejea kimeo.
*_BY OCHU_*
*_mfungwa huru_*
Saturday, March 3, 2018
WARINGAO
Muringao matajiri, mukafurahia mali.
Akujieni fakiri, mwamsukumia mbali.
Hili jambo sio zuri, zikumbukeni asili.
Hakuna mkamilifu, waringao nawambia.
Waringao kwa viriri, kutoa sauti kali.
Mengi wanayahubiri, kutekeleza muhali.
Kwao waona fahari, ila kwetu idhilali.
Yaepukeni machafu, unafiki punguzeni.
Waringao kwa uzuri, umbo na sura jamali.
Wakavifanya viburi, wengine kuwadhalili.
Wajue kuna hatari, wasisahau ajali.
Hakuna mkamilifu, waringao nawambia.
Muringao nyie wari, akija mume kikweli.
Mnayapinga mahari, sababu za kijahili.
Muko radhi takriri, zinaa iwe amali.
Yaepukeni machafu, waringao nawambia.
Waringao kwa umri, pumzi za mola jalali.
Leo nawatahadhari, yatie kwenye akili.
Kuna siku itajiri, kutengwa roho na mwili.
Hakuna ataebaki, waringao nawambia.
Litaendelea
By Othame
Mfungwa huru
Muringao matajiri, mukafurahia mali.
Akujieni fakiri, mwamsukumia mbali.
Hili jambo sio zuri, zikumbukeni asili.
Hakuna mkamilifu, waringao nawambia.
Waringao kwa viriri, kutoa sauti kali.
Mengi wanayahubiri, kutekeleza muhali.
Kwao waona fahari, ila kwetu idhilali.
Yaepukeni machafu, unafiki punguzeni.
Waringao kwa uzuri, umbo na sura jamali.
Wakavifanya viburi, wengine kuwadhalili.
Wajue kuna hatari, wasisahau ajali.
Hakuna mkamilifu, waringao nawambia.
Muringao nyie wari, akija mume kikweli.
Mnayapinga mahari, sababu za kijahili.
Muko radhi takriri, zinaa iwe amali.
Yaepukeni machafu, waringao nawambia.
Waringao kwa umri, pumzi za mola jalali.
Leo nawatahadhari, yatie kwenye akili.
Kuna siku itajiri, kutengwa roho na mwili.
Hakuna ataebaki, waringao nawambia.
Litaendelea
By Othame
Mfungwa huru
Mashairi
1)SILAZIMISHI
Sitalazimisha katu, jembamba likawa nene.
Sitakuwa mtukutu, ukaidi niufane.
Tautunza wangu utu, hata nyinyi mnikane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Sitokivaa kiatu, pia huku kinibane.
Silazimishi papatu, miguuni kinichaane.
Siutaki ukurutu, nyayo jasho ziroane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Siwi kama mbwa mwitu, m-babe nionekane.
Jamii mambo na watu, sote tushirikiane.
Siwalazimishi katu, matusi msitukane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Mimi mtu kama watu, heshima tuwekeane.
Sitalazimisha katu, mimi nawe tufanane.
Katuumba mola wetu, ili tusaidiane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
By ochu
Mfungwa huru
2)WANATAMANI NIZIKWE
Dunia ni mtihani, na ina mengi maafa.
Inanitia huzuni, macho yamefanya nyufa.
Watu Kama mashetani, nyoyo zao si nadhifa.
Ipo siku nitakufa, nakuzikwa nitazikwa.
Kwa nini mnatamani?, nizikwe bado sijafa.
Au nimekosa nini?, nikashusha zenu sifa.
Yenu madonge rohoni, yatatibia kifafa.
Ipo siku nitakufa, nakuzikwa nitazikwa.
Asiyekosa ni Nani?, akawa ja malaika.
Inanitia huzuni, makosa kunilimbika.
Nitazikwa kaburini, siku yangu ikifika.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Siijui siku gani, nukta saa na dakika.
Wala sina upinzani, duniani tatoweka.
Kinafiki buriani, machozi yatawatoka.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Ala moja asilani, hazikai panga mbili.
Nitakufa pasi shani, wakati kafa rasuli.
Namuomba rahmani, nife huku nikiswali.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Beti sita za huzuni, sitaki nifike mbali.
Kufa kikondoo kwani, kiungwana nakubali.
Mito hwenda baharini, wanadamu kwa jalali.
Nanyi pia mtakufa, na kuzikwa mtazikwa.
_*Ochu*_
_*Mfungwa huru*_
Sitalazimisha katu, jembamba likawa nene.
Sitakuwa mtukutu, ukaidi niufane.
Tautunza wangu utu, hata nyinyi mnikane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Sitokivaa kiatu, pia huku kinibane.
Silazimishi papatu, miguuni kinichaane.
Siutaki ukurutu, nyayo jasho ziroane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Siwi kama mbwa mwitu, m-babe nionekane.
Jamii mambo na watu, sote tushirikiane.
Siwalazimishi katu, matusi msitukane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
Mimi mtu kama watu, heshima tuwekeane.
Sitalazimisha katu, mimi nawe tufanane.
Katuumba mola wetu, ili tusaidiane.
Cha kwangu hakiwi chako, mola ndie mpangaji.
By ochu
Mfungwa huru
2)WANATAMANI NIZIKWE
Dunia ni mtihani, na ina mengi maafa.
Inanitia huzuni, macho yamefanya nyufa.
Watu Kama mashetani, nyoyo zao si nadhifa.
Ipo siku nitakufa, nakuzikwa nitazikwa.
Kwa nini mnatamani?, nizikwe bado sijafa.
Au nimekosa nini?, nikashusha zenu sifa.
Yenu madonge rohoni, yatatibia kifafa.
Ipo siku nitakufa, nakuzikwa nitazikwa.
Asiyekosa ni Nani?, akawa ja malaika.
Inanitia huzuni, makosa kunilimbika.
Nitazikwa kaburini, siku yangu ikifika.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Siijui siku gani, nukta saa na dakika.
Wala sina upinzani, duniani tatoweka.
Kinafiki buriani, machozi yatawatoka.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Ala moja asilani, hazikai panga mbili.
Nitakufa pasi shani, wakati kafa rasuli.
Namuomba rahmani, nife huku nikiswali.
Ipo siku nitakufa, na kuzikwa nitazikwa.
Beti sita za huzuni, sitaki nifike mbali.
Kufa kikondoo kwani, kiungwana nakubali.
Mito hwenda baharini, wanadamu kwa jalali.
Nanyi pia mtakufa, na kuzikwa mtazikwa.
_*Ochu*_
_*Mfungwa huru*_
Subscribe to:
Posts (Atom)