Monday, March 12, 2018

BILA WEWE

Yaani wewe!, Uliyefanya jina langu likatukuka.
Si mwenginewe, uniokotae pale ninapoanguka.
Na *_bila wewe_*, duniani daima nisingetambulika.


Ndie wewe!, uliyenifanya Tungo nikaiandika.
Si mwenginewe, ila wewe ubongo wangu umeuteka.
Na *_bila wewe_*, furaha yangu duniani ingetoweka.


Haswa! Wewe,  uyakosapo mafuta maji hunipaka.
Huna kiwewe nikikukosa hujawahi kasirika.
Na _*bila wewe*_, tabu nyingi nayo mashaka yangenifika.


Ibaki wewe, ninapotukanwa moyo wako huungulika.
Sifa upewe, hujawahi nibagua katika kila rika.
Na *_bila wewe_*, nisingelijua lipi jema la kushika.


_*by Ochu*_

_*Mfungwa huru*_

No comments:

Post a Comment