_*UMOJA*_
Wahenga walichonena, umoja huwa ni nguvu.
Na walileta maana, umoja sio uchovu.
Sasa wengi wamenuna, wamevimbwa na mashavu.
Umoja nguvu daima, ikiwa mutapatana.
Mali huzichuma wote, wakubwa wadogo pia.
Si lolote si chochote, wadogo wadhulumiwa.
Pia bado waufyate, bila ya kujitetea.
Umoja nguvu daima, ikiwa mutapatana.
Usikubali dhuluma, mola ametuambia.
Jiepushe himahima, dhulumiwa dhulumia.
Wala usikate tama, chako halali pania.
Umoja nguvu daima, ikiwa mutapatana.
Mukiwa na moja lengo, dhamira na moja nia.
Mukaipanga mipango, mbali mutajifikia.
Mutakwenda songombingo, pale mukijibagua.
Umoja nguvu daima, ikiwa mutapatana.
Ukiwa u umojani, hasara itatufika.
Ila ukiwa makini, utabaki nufaika.
Huu si wa Marekani, ni wa hapa Afirika.
Umoja nguvu daima, ikiwa mutapatana.
_*Mfungwa huru*_
No comments:
Post a Comment