Monday, April 9, 2018

_*MAWAZO*_

Asubuhi na mapema, naamka nikiwaza.
Kwamba lini nitasoma, niondokane na kiza.
Nikapatwa na muhuma, kwa sana kuwazawaza.
Mawazo ya akili, fakiri ndipo utende.


Siku nyengine hawaza, wapi tapata elimu?.
Nikaenda kuuliza, nikambiwa mwendazimu.
Mbele kukatanda kiza, kanitoka yangu hamu.
Mawazo ya akilini, fakiri ndipo utende.


Siku nenda siku rudi, wazo langu hurejea.
Nikaifanya juhudi, elimu 'jitafutia.
Nikamuomba wadudi, kweli kanisaidia.
Mawazo ya akilini, yanaweza kuwa sawa.


Nikaipata elimu, ya akhera na dunia.
Sasa naitwa mwalimu, kwa wazo lofikiria.
Kumbe mawazo matamu, yale yalio sawia.
Mawazo ya akilini, mengine huwa mazuri.


Kuna mawazo mabaya, mengine hujitokeza.
Hukupeleka kubaya, hukugubika na kiza.
Jiepushe hima haya, uepuke hiyo adha.
Mawazo ya akilini, kuwaza na kuwazua.


_*Mfungwa huru*_

No comments:

Post a Comment