Monday, April 9, 2018

*_UKALI WAKE PORINI_*🐆🐆


Kuna mapori sahali, katika mbuga na nyika.
Yaliyojitenga mbali, kisehemu na mipaka.
Muna wanyama wakali, na wanaoyayatika.
Ukali wake porini, vinyama vyasulubika.


Simba dume mfalume, katika pori la taza.
Wala hanacho kimeme, njaa inapomkwaza.
Mbioze Kama umeme, paa swala hufukuza.
Ukali wake porini, vinyama vyasulubika.


Pori la zaza nakama, iliwapata zamani.
Maji wanaita mma, malkia kawa duni.
Inapokuja neema, Simba dume huja ndani.
Ukali wake porini, vinyama vyasulubika.


Sautile kama radi, chini inapoanguka.
Vitimbi na zake kedi, vinyama vinasumbuka.
Ubaya zake hasadi, malkia kamchoka.
Ukali wake porini,  vinyama vyasulubika.


Kukimbia hawawezi, digidigi nyani pia.
Wanamuomba mwenyezi, shufaa kuwapatia.
Simba dume kawa chizi, kutwa anawavamia.
Ukali wake porini, vinyama vyasulubika.



BY OCHU

_*MFUNGWA HURU*_

No comments:

Post a Comment