Monday, April 9, 2018

***MWALIMU***
1)Kilio changu natoa, sikieni nyi kaumu. Hakuna wakukosoa, nayasema mufahamu. Si dibeti nawambia, na mdahalo haramu. Mwalimu athaminiwe, hadhiye iyonekane.
2)Jukumule mwatambua, akifika skulini, darasani huingia, vipindivye kwa foleni, mwili umejichokea anaporudi nyumbani. Huruma namuonea,
hali yake taabani.
3) Arudiapo nyumbani, bado huwa yu kazini. huziandaa lesani, japo nyinyi hamuoni. kweli yuko mashakani, kitanda hakitamani.  athaminiwe mwalimu, hadhiye iyonekane.

4)Mwalimu yeye ndo chanzo, maendeleo nchini. mwalimu ndie kigezo, kwa walio darakani. yeye kawapa mafunzo, walipokua shuleni. Mwalimu athaminiwe, hadhiye iyonekane
5)Mafunzo
mzo kwa mzo, walipatiwa yakini. daktari acha bezo,injinia kaa chini. vikosi siwe gumzo, mwalimu mkamuhini.bila yeye asilani, musengefika mulipo.
6) mshahara wake duni, laki mbili thamanini. hununulia sabuni, chakula hakuna ndani, tarehe pili mwezini, anakopa kwa jirani. mwalimu athaminiwe hadhiye iyonekane.


   Mfungwa huru

No comments:

Post a Comment