TUNAKWENDA MRAMA
Chombo chaenda mrama, angalieni
Tulipotoka,tulipo na tuendako
Kina cha maji chapanda.
Na nahodha akasema, takulindeni, tutaokoka, katika misukosuko , pasi na tanga kutanda.
Tunasonga ma!ma!ma!ma!, mkondoni,
Tunateseka, nahodha toa tamko,
'Tafika tunapokwenda.
Tunakwenda mrama, tuunganeni,
Kunusurika, katika mahangaiko,
Tufike tunakokwenda.
Nahodha huyu si mwema, tumsuteni,
Mwema kuweka, asio na chokochoko,
Afueni itatanda.
By ochu
Mfungwa huru
No comments:
Post a Comment