Monday, April 9, 2018

_*NILIPOKUFATA*_

Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.
Nilizani utakwenda, pale nilipokuita.
Kwani ulikuwa nyonda, sura yako sinyorita.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_


Nilikuona mcheshi, mwenye tabasam pia.
Sikukwambia uzushi, yale yanonisumbua.
Nawe hukuwa m-bishi jibu zuri ukatoa.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_


Moyo wangu ulipenya, kwenye zote chemba zako.
Na wewe uliniponya, kwa zuri lako tamko.
Niliruka kama panya, kwa furaha na kicheko.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_


Nakupenda peke yako, hili halina utata.
Nikikosa pendo lako, duniani nitajuta.
Nipende bila vituko, waseme wanaobwata.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_


*_by Ochu-mimi_*

_*Mfungwa huru*_

No comments:

Post a Comment