_*NILIPOKUFATA*_
Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.
Nilizani utakwenda, pale nilipokuita.
Kwani ulikuwa nyonda, sura yako sinyorita.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_
Nilikuona mcheshi, mwenye tabasam pia.
Sikukwambia uzushi, yale yanonisumbua.
Nawe hukuwa m-bishi jibu zuri ukatoa.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_
Moyo wangu ulipenya, kwenye zote chemba zako.
Na wewe uliniponya, kwa zuri lako tamko.
Niliruka kama panya, kwa furaha na kicheko.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_
Nakupenda peke yako, hili halina utata.
Nikikosa pendo lako, duniani nitajuta.
Nipende bila vituko, waseme wanaobwata.
_*Moyo wangu ulidunda, mwanzo nilipokufata.*_
*_by Ochu-mimi_*
_*Mfungwa huru*_
No comments:
Post a Comment