Monday, April 9, 2018

_*KIMWANA UMENIWEZA*_

Acha leo niyanene,  maneno kukuambia.
Midomo nisiibane, utumu menikolea.
Moyo Uwachwe sonone, wazi nakumtamkia.
Kwa kweli umeniweza, penzi limenikolea.


Mitego yako sikane, mpenzi wanijulia.
Lengo lako unibane,  nisije kukukimbia.
Menifanya nisione, kipofu kwako tambua.
Kikweli umeniweza, penzi limenikolea.


Sijui kipi ninene, Utamu menizidia.
Pasua moyo uone, peke yako umekaa.
Njoo basi nikukune, penzi lizidi kumea.
Kimwana umeniweza, kukuwacha sijawaza .


_*Mfungwa huru*_

No comments:

Post a Comment