Monday, April 9, 2018

_*KIINI MACHO*_


itatufika hasara, tukiwa twayapuuza.
Tupaparike papara, kabla kuingia kiza.
Kiona miji yang'ara, ujuwe waning'ariza.
Tutabaki kushangaa, mazuri ughaibini.


Kiini macho wabunge, mawaziri natuhumu.
Twanyanyasika wanyonge, kwetu maisha magumu.
Wanazila zetu tonge, wamenogewa utamu.
Tutabaki tu kuimba, maisha bora nchini.


Sheria kwetu WA chini, ndio tuliotungiwa.
Walo juu kiririni, kiwabana hupinduwa.
Kiini macho machoni, hivihivi twaibiwa.
Tutabaki tu kuimba, sote chini ya sheria.


Si kesi mahakamani, mfungwa huru najua.
Mengi huwa natamani, ndo mana nayasemea.
Hongo zao kibindoni, ndizo zinotununua.
Tutabaki tu kuimba, rushwa adui wa haki.



_*Mfungwa huru*_

No comments:

Post a Comment