Friday, May 31, 2019

SHAIRI: LAKINI?

*_LAKINI!_*

Sauti yangu napaza, isikike hadharani
Mema nikiyatangaza, na mabaya kubaini
Lakini! sitaki kwaza, Mfungwa si kifungoni


Barabara zipo nyingi, mijini na vijijini
Hili jambo silipigi, jitihada nabaini
Lakini! ajali nyingi, twapinduka mashimoni


Maji Safi na salama, twayapata majumbani
Bomba zisambaa vyema, zimeungwa kwa makini
Lakini! metuandama, tulipe mwisho mwezini


Elimu inapepea, imekuwa afueni
Watoto wajisomea, bure tena kwa amani
Lakini! najionea, mwalimu hali ni duni


_*Litaendelea*_

_*Lakini! Sijui lini!*_


_*Mfungwa huru*_
othame10@gmail.com

No comments:

Post a Comment