Saturday, October 12, 2019

MJUE MFUNGWA HURU

MJUE OTHMAN AME HAMZA (MFUNGWA HURU) KUPITIA MAHOJIANO HAYA YALIYOFANYIKA KATIKA KUNDI LA WASAP LIITWALO MALENGA CHIPUKIZI (12/9/2019)

ABU HAYTHAM: πŸŽ™πŸŽ™πŸŽ™
Bwana Othman, karibu katika studio zetu za Malenga Chipukizi, karibu ukaribie

Mfungwa huru: 
Shukran nimekaribia

ABU HAYTHAM: Assalaamu alaykum alhabeeb, wajionaje na hali?

Mfungwa huru: Waalaykum salam, Hali yangu iko vyema alhamdulillah

ABU HAYTHAM: Mkeka upo, kama wahisi kiti hakikupi utulivu tuketi mkekani

Mfungwa huru: πŸ˜‚πŸ€£ panatosha kitini

ABU HAYTHAM: Maa shaa Allaah! Nadhani wana malenga wanakufuatilia kwa karibu kabisa. Hebu jitambulshe walau kwa muhtasari

Mfungwa huru: Naam, Jina langu ni Othman Ame Hamza, kwa jina la lakabu ni Mfungwa huru... Mzaliwa wa Donge, Unguja Zanzibar na ndipo makaazi yangu kwa sasa

ABU HAYTHAM: Aywaa, labda tuanze hapo kwenye lakabu ya "Mfungwa Huru". Ilikuwaje na ufungwa wa uhuru alhabeeb?

Mfungwa huru: Ah! Jina hili linatokana na shairi langu ambalo binafsi nililipenda sana, mwanzo wa shairi hilo nililipa anuani "wafungwa huru" lakini nikahisi nikitumia nafsi ya umoja litakaa vizuri... Kwa hiyo jina linatoka hapo, ilikuwa kama ilhamu tu

ABU HAYTHAM: Marhabaa, hili ni shairi lako la kwanza au la ngapi kama unakumbuka?

Mfungwa huru: Kiukweli siyo la kwanza, nilishawahi kuandika mashairi matano kabla ya hili,

ABU HAYTHAM: Safi sana, tuhame huku kwanza tutarudi baaden.

Kwanza kwa niaba ya wafuatiliaji nikupongeze sana kwa kuanzisha ukumbi huu. Mola akulipe kila la kheri

Mfungwa huru: Amiin, kwa sote insha Allah

ABU HAYTHAM: Na natazama tarehe, yaonesha mwezi ujao ukumbi huu utakuwa unatimiza miaka miwili kamili.

Labda ulisukumwa na nini na ulifikiria nini hadi ukaanzisha ukumbi huu adhimu?

Mfungwa huru: Ahaa! Historia ya ukumbi huu ni kubwa sana,
Tulipokuwa chuoni SUZA kulikuwa na kundi la NKURUMAH DEGREE EDUCATION sisi wapenzi wa mashairi kipindi hicho tulikuwa tunatuma kazi zetu huko, Ila baadhi ya watu hawakufurahishwa, hapo tukashauriana Mimi na bwana Abdillah Mohammed (Mcheza kwao) tuanzishe kundi la mashairi kwa ajili ya darasa letu , tulikubaliana tukaanzisha kwa ajili ya NKURUMAH tu pekee kwa wakati huo.Baadae tukalenga kwa ajili ya Wanafunzi wa Zanzibar tu hata kama wanasoma nnje ya Zanzibar, lakini Mambo yaliponoga na kupata watu wengi zaidi kwa sasa ni kundi lenye malengo makubwa zaidi ya hayo ya awali, naweza kusema kikundi kimekuwa

ABU HAYTHAM: Naam, Ni kweli, sasa kimekusanya wengi wasomao na wafundishao

Mfungwa huru: πŸ€£πŸ˜‚πŸ˜‚naam

ABU HAYTHAM: Unajiskiaje unapoona huu ukuaji wa kikundi?

Mfungwa huru: Napata faraja sana, na hupenda watu wakiingia humu hata kama hawatungi basi wasitoke, muhimu ni kuwekeana heshima tu baina yetu, pia tuwe na dira na malengo yanayofanana

ABU HAYTHAM: Hakika!
Bwana Othman nakufahamu kama mshairi, bila kujali kiwango chako na vyovyote ujiitavyo.
Wafuatiliaji wanapenda kujua, je katika familia yenu kuna asili ya ushairi? Yaani kuna mtu yeyote katika familia alikuwa ni mshairi?

Mfungwa huru: Dah! Sina uhakika na sikumbuki kama nyumbani palitokea mshairi, Ila Nina mjomba ambaye anatunga tenzi hasa za sherehe za maulidi, na za kichama

ABU HAYTHAM: Alaa, unataka kusema kuwa mjomba ni moja ya watu waliokuvuta ushairini?

Mfungwa huru: Nathubutu kusema hivyo,

ABU HAYTHAM: Au kuna wakongwe wengine waliokuvuta?

Mfungwa huru: Unajuwa Mimi ni mpenzi wa mashairi tangu nikiwa mdogo bila kujijuwa, nilipenda sana kusoma qaswida nilipokuwa madrasa, Sasa tukipata mialiko baadhi ya madrasa pia huzisikia tenzi za mjomba zikaghaniwa, nilikuwa napenda sana, Na kipindi hicho ilikuwa sijui chochote kuhusu ushairi,

ABU HAYTHAM: Vyema sana, naweza sema ushairi umeshapenya damuni mwako.

Pengine twataka kujua, shairi la kwanza ulilitunga lini na linakwenda na maudhui gani?

Mfungwa huru: Swali hili linanipa kigugumizi kidogo,
Ila Shairi langu la kwanza nililitunga nikiwa kidato Cha nne, lilihusu elimu (sikulihifadhi kwa njia yoyote)

ABU HAYTHAM: Oh! Pole sana

Mfungwa huru: Ahsante

ABU HAYTHAM: Napata nyepesinyepesi kuwa una diwani ipo sokoni, hili lina ukweli wowote?

Mfungwa huru: Diwani zipo, alhamdulillah,

ABU HAYTHAM: Kwani zipo nyingi?

Mfungwa huru: Zipo 2,

ABU HAYTHAM: Sawa, labda tujaalie majina na zinauzwaje?

Mfungwa huru: Diwani ya kwanza nilishirikiana na Washairi watatu Binti bogoyo, Mcheza kwao, na mwalimu NAM ambayo inaitwa MALENGA WA ZENJI Nna ya pili ambayo imetushirikisha Wanafunzi wengi kutoka SUZA inaitwa KILINGE CHA UKOMBOZI, zote hizi zinauzwa kwa shilingi 8000 tu za Kitanzania.

ABU HAYTHAM: Maa shaallah. Othman, katika vitu ambavyo husemwa kuhusu uandishi hasa wa mashairi ni kwamba washairi ni watu duni na pia ushairi ni wa wazee. We walionaje hili, au hujawahi kukutana nalo?

Mfungwa huru: Kuhusu ushairi ni wa wazee sijawahi kukutana nalo, Ila kuhusu Washairi ni watu duni hasa kimaisha tayari nimeshakutana nalo

ABU HAYTHAM: Umesema kuwa washairi ni watu duni sana hasa kimaisha, na umekiri kukutana na jambo hili. Umekutana nalo wapi?

Mfungwa huru: Kwanza nakiri kwa kulisikia midomoni mwa watu wengi, haswa washairi wenyewe... Pia Kuna ushahidi nachelea kuutoa, lakini wacha nikate jongoo kwa meno... Mfano mshairi Haji Gora ukifuatilia hadhi yake kimashairi na maisha yake ni vitu viwili tafauti na sio huyo tu ata Washairi wengine 

ABU HAYTHAM: Alaa

Mfungwa huru: Naam

ABU HAYTHAM: Ni kweli yasikitisha, na mfano wako wasemwa na wengi. Labda wewe kama mshairi unayekuja kwa kasi, unadhani hili litapunguaje hadi tuseme limekwisha?

Mfungwa huru: Dah! Umenikweza Sana, Ila kupunguwa kwake kwanza washairi tuwe kitu kimoja, tuungane mkono katika kazi zetu ambazo tunazifanya, pia kutetea maslahi yetu kwa pamoja... Kwa namna yoyote ile hata kama kwa kuanzisha jumuiya na vyama vyenye kusimamia washairi

ABU HAYTHAM: Nimekupata sana...

ABU HAYTHAM: Kila msanii huwa ana kiigizo, wazungu wanasema Role Model. Siamini kama wewe huna, tujaalie tumjue umuigaye au utamaniye kuwa kama


Mfungwa huru: Natamani kuwa Kama wengi tu, Mimi washiri wengi natamani kuwa Kama wao. Kuhusu nimuigae, nawaiga wengi pia

ABU HAYTHAM:
Wakati unaanza ushairi, lazima kuna washairi wakubwa wa kale ulikuwa ukiwapenda au hata sasa ujiendelezavyo kwa kusoma kazi zao unakiri ukongwe wao na ubobevu fanini.

Usitukatili, tutajie ili pengine nasi tujikongojao tunaweza kufukua kazi zao na kustaladhi kama wewe. Sogea karibu ya kipaza sauti, naona sauti yako imekuwa hafifuπŸŽ™

Mfungwa huru: πŸ€£πŸ˜‚sawa, Kama nlivyosema awali kuwa nlikuwa naupenda ushairi tangu zamani lakini sikujuwa nini hasa ushairi, nilipokuwa kidato Cha tatu baada kusoma vitabu vya Malenga Wapya na Wasaka Tonge vilinivutia sana, naweza kusema wenye vitabu hivi kwangu ulikuwa ni mfano wa kuwaiga, lakini kila nilipojifunza nilikutana na wengi zaidi ya hao,

 ABU HAYTHAM: Sawa sawa...

Labda tuambie lini hasa uliona kuwa ushairi unaanza kukukubali na kwa hilo ukaazimia kutouacha?

Mfungwa huru: Baada ya Kutunga Shairi la "Mfungwa huru" mwaka 2017 Kama mwezi wa 9 hivi,

ABU HAYTHAM: Baada ya kipindi tutakuomba utuoneshe ili nasi tuhamasike, tuelimike na tuburudike

Mfungwa huru: Kwa wale wenye nakala za Malenga wa Zenji Shairi linapatikana humo, lakini pia nitalituma, usijali

ABU HAYTHAM: Naomba kwa ridhaa yako, niruhusi maswali mawili kutoka kwa wasikilizaji
Kabla sijamaliza kwa maswali mawili ya mwisho

Mfungwa huru: Wasikilizaji na watazamaji karibuni

BONGO TATA: Mzee mimi kwanza ameoa na kama ameoa kivip anweza kudhibiti mda wa ndoa na sanaa

Mfungwa huru: Jawabu ni fupi tu,,, bado sijaoa

ABU HAYTHAM: Tunashukuru, maana yake na swali la pili limekufa kifo cha kawaida...

ABU HAYTHAM: Nafasi ya mwisho kwa mfuatiliaji mwingine...

ABU HAYTHAM:Tumalize, kwa kukushukuru sana kwa muda wako.
Tunakuomba tu utustahmilie na utuwie radhi. Tupigie picha shairi lako la Mfungwa Huru kutoka katika diwani tajwa
 Na utueleze kuwa diwani yako inapatikanaje kwa mwenye kuihitaji

Mfungwa huru: Kwa Sasa hapa nilipo sina nakala, ipo sehemu nyengine, Ila nitatumia njia nyengine mtalipata
 Diwani kwa Sasa kwangu  kopi zimemaliza, labda kwa Mcheza kwao au binti bogoyo Kama zipo,

ABU HAYTHAM: Tafadhali Bwana Othman kwa muda wako na ninakushukuru sana, malizia kahawa yako na nikutakie usiku mwema

Mfungwa huru: Ahsante, shukrani na wewe pia

No comments:

Post a Comment