*_LAKINI!_*
Sauti yangu napaza, isikike hadharani
Mema nikiyatangaza, na mabaya kubaini
Lakini! sitaki kwaza, Mfungwa si kifungoni
Barabara zipo nyingi, mijini na vijijini
Hili jambo silipigi, jitihada nabaini
Lakini! ajali nyingi, twapinduka mashimoni
Maji Safi na salama, twayapata majumbani
Bomba zisambaa vyema, zimeungwa kwa makini
Lakini! metuandama, tulipe mwisho mwezini
Elimu inapepea, imekuwa afueni
Watoto wajisomea, bure tena kwa amani
Lakini! najionea, mwalimu hali ni duni
_*Litaendelea*_
_*Lakini! Sijui lini!*_
_*Mfungwa huru*_
othame10@gmail.com