_*NUSU ZUZU,NUSU ZEZETA*_
Akili nusu zezeta, nusu imekuwa zuzu, umeizuzua
Mwili umenizorota, mwembamba kama kauzu, umejikondea
Moyo unanitukuta, tuu! tuu! unajuzu, umeuonea
Miguu hafurukuta, imeingia kibibi, haina hisia
Tumbo linanisokota, umeisha ujanabi, umeshakimbia
Leo hii wanisuta, huniti tena hababi, yako kutumia
Huba kwako limekata, thamani 'mepukutika, ulonipatia
Kuna jambo ulifata, leo umenifutuka, hukua na nia
Ipo siku nitapata, mrembo kukufunika, alietimia
Uchungu umenipata, hadi haya kuandika, jua naumia
Shauri tulolikata, kuwa sote tutafika, hadi kwenye ndoa
Ni ruya yenye utata, na zuzu nimezuzuka, bora kujifia
Funzo nimeshalipata, kwako nilifanya kosa, sitalirejea
Nenda na mimi 'tapata, mzuri asie visa, na mbaya tabia
Amba mimi ni zezeta, na zuzu mtoa pesa, niko safi nia
_*Othman Ame Hamza*_
*_Mfungwa huru_*
0776820608
othame10@gmail.com