HUSDA
1. Macho yangu nayalenga, kwako wewe mwanadamu
Unokwenda kwa waganga, mwengine kumdhulumu
Tena mipango wapanga, hata kwa kumwaga damu
2. Husda imejikita, imo kwenye yako damu
Ya kheri yanakupita, wakumbatia haramu
Kulala wasitasita, wakesha kwenye mizimu
3. Lengo yeye vimtoke, kuwa navyo huna hamu
Watoto na mali zake, vyote unavihujumu
Utu na thamani yake, kwake iwe ni hatamu
4. Mwanaadamu zinduka, husda siyo muhimu
Tujiepushe haraka, tabia hii ni sumu
Akhera tutapofika, Kuna moto Jahanamu
Kiitikio
Husdaa... Husdaa... Husdaaa... Kwetu hatari
Husdaa... Husdaaa.... Husdaaa.. tujihadhari