Kilinge Cha Ukombozi ni kitabu cha Mashairi kilichotungwa na washairi chipukizi pia wakiwa ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Mawazo ya kuandikwa kwa Kitabu hiki yametoka kwa uongozi wa CHAWAKAMA-SUZA wa mwaka 2018/2019 ukiwa chini ya mwenye kiti Abdillah Mohammed Kassim (Mcheza kwao). Wazo Hilo liliwafikiwa na kuratibiwa kwa ajili ya kuazisha shindano mbalo lingewezesha kupatikana kwa Mashairi hayo. Mashairi hayo yalikusanywa na mhariri mkuu ndg. Othman Ame Hamza (Mfungwa huru) kwa ajili ya kupata washindi. Kwa kuwa washiriki walikuwa wengi washairi 25 wa mwanzo walibahatika kuingizwa pamoja na viongozi 10 waliotunga Mashairi yao hapo awali. Kitabu hiki kimehaririwa kwa ustadi na umahiri mkubwa na Dkt. Omar Salum Mohamed na kuchapishwa kwa mara ya kwanza na Mwimbe Priters iliyopo Bagamoyo mwaka 2019. Kuandikwa kwa kitabu hiki kumetokana na sababu nyingi.
Kwanza, kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili,
Pili, kuendeleza na kukuza vipaji vya washairi hasa chipukizi
Tatu,kuchochea uwandishi wa kazi za kifasihi hasa kwa upande wa Zanzibar.
Nne kuhifadhi na kulinda utamaduni wa Mswahili.